Psalms 114:1-6

Maajabu Ya Mungu Wakati Israeli Walipotoka Misri

1 aWakati Israeli walipotoka Misri,
nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 bYuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu,
Israeli akawa milki yake.

3 cBahari ilitazama ikakimbia,
Yordani ulirudi nyuma,
4 dmilima ilirukaruka kama kondoo dume,
vilima kama wana-kondoo.

5 eEe bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,
nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume,
enyi vilima, kama wana-kondoo?
Copyright information for SwhNEN